Thursday, August 23, 2012

SUBIRA HUVUTA KHERI


Kheri huletwa na mwenyezi mungu,mwanadamu ana kheri ya kuwa na pumzi ambayo humfanya akaweza vile awezavyo kwa Kheri yake Muumba,unaweza kusubiri  mpaka tumbo likauma mambo mengine hayana subira,mwanzo ukiwa mgumu haimaanishi kwamba mwishoni ni neema ikawe kwa subira na kuupoteza muda,pengine usipojua subira nyingine bado hazijafanyika,unaweza kupoteza ukisubiri tena sio sana ama ikawa kheri kwa kuwa mmoja alisubiria,leo upoteze vurugu kwa kuwa na subira,usiseme tu kama iwavyo kwa dalili ya mvua,labda ukiwa unahitaji mazao mengi kwa pale ulipoandaa shamba lako

Iwapo kusema kabla ya tendo ni dhambi na uongo usingekuwepo,dhambi nyingi tu.
usisubiri ufike muda ili uanze kudanganya vyema,haina budi kusubiria maisha na kusema Mungu atakupa,hii ikiwa wewe ndiye unaye yaendesha maisha yako kwa kuwa Kheri ulishapewa,kuendesha taratibu ni sawa na kumsubiri abiria wakati wengine wanaharaka,hivyo bora utumie mwendo kasi unaokufaa, kama umechelewa utaenda na usafiri mwengine,uyape majina na rangi ili uweze kujua,kuwepo na subira zako za kutaka kuona na kujua,vingine ukiwa na subira za kutaka kuyaona maisha magumu yako wapi kwa udanganyifu wa kulipia subira pamoja na manung'uniko.

Huu ni mwanzo,sijui unaishi unategemea kufika mpaka mwisho upi,ama unaishi kusema kwamba leo au kesho kitalika nini,pamoja na ada ya watoto,si shule tu maana hata pumzi inalipiwa siku zote.kwa walio wengi wanajua kile wanachokitafuta maana kila aliye na chake akitumie,ikiwa ni macho kuona ama akili kufikiri,mengi yanatokana ikiwa umeamua mwenyewe kufanya,yaani ni unataka nini  maishani mwako,pengine ndiyo mlengo wa maumbo na thamani tofauti tofauti,na hivyo hauzaliwi navyo ukavikuta zaidi ya kusubiri na kuona yanayojiri,pengine haina haja ya kusubiri ikiwa yanayojiri yanaletwa na wewe wenyewe.

Saturday, August 18, 2012

VYOMBO..


Vingine vikiwa vinaleta habari na vengine vikiwa na kutumika kutokana na matumizi yake,hata habari ni matumizi maana imetumika kupitia hivyo,ikiwa kuna waheshimiwa wanahaki ya kuonekana katika vyombo hivyo,ikiwa ni majanga ama iwe ni namna yoyote ya kumtaka mwanadamu aweze kupata ufahamu,ufahamu ni jambo jema sana na kwa Yule anayefahamishwa ameelewa,maana ni lazima uelewe hata ya kuwa haukupanga kuelewa,hizi ni bidhaa,kuanzia pale inapoanzwa kutengenezwa mpaka inapofika,bidhaa mara nyingine huwa zinamtindo wa kuchacha na baadaye kuharibika ikiwa ni mwisho wa matumizi ya bidhaa hiyo,ni haki lakini ni dhahma kwa lile linaloendelea na kutaka faida wakati bidhaa kiujumla zimechacha,tutaharibiana matumbo hata kama ni wazi tuna njaa ya siku tatu.hazipaswi nyingine kukaa katika vyombo vya habari.

Leo utasikia waziri kafanya hili na kesho tusisikie nabii kafanya nini,hili linaashiria kutokufanya kwamba,haimaanishi watu wanakwepa majukumu yao ama vile ilivyo kwa upendeleo,hii ni namna ya vyombo vilivyoelekezwa ni vipi viweze kubeba chakula,maji,maono na masomo,pengine ikiwa kama abiria katika usafiri,na kama itatokea ajari basi hapa ndiyo tutaizungumzia yaliyojiri,vyombo vikiwa na mlengo zaidi wa mwenye chombo kuliko Yule anayeuziwa bidhaa,ama  kweli hii ni biashara,ingawa haina maana ya kushangaa,pengine ikiwa mambo ni baadhi ya yaliyopo katika chombo kilichotubeba.

Dunia ikiwa kama ni chombo mahususi ambacho kimsingi tumeweza kuwa humo,kama kutumika mpaka tunaisha,mara nyingi vyombo ni vile tunavyokuwa navyo ama tunavyoviacha baada ya sisi kuwa na hitaji la namna nyingine,pengine ikiwa .pengine tuangalie kile tunachokiweka katika chombo ali mradi kikakaa vyema,pengine hata jamii ikaelewa kama sio kueleweshwa,maana kwa vyombo vingine hata kama vimejaa watu wanapanda tu,bila kujua chombo chenyewe hakisemi,vingine hivi tunavyowaandika watu ili taarifa ziwafikie zisiwe kumchafua ali mradi ukauza,maana hao wanaochafuka wakiamua kuchafua kweli inawezekana kukosa hata mahala pa kuziweka bidhaa,ama na wao wauze hata  bidhaa zikawa hakuna.abiria jichunge..mizigo haibebwi.

Friday, August 17, 2012

MAISHA YAKO....

The purpose of life is not to be happy – but to matter, to be productive, to be useful, to have it make some difference that you have lived at all.
       
Leo Rosten, American teacher and humorist

Yaweza usitegemee yakuwa haijatokea katika maisha yako,usimtegemee mtu yoyote katika maisha yako hii ikiwa ni kauli ambayo inahitaji mtu kujiamini,kujipa nguvu na sio chuki ya kujitenga,kufikiri na kujua kama maisha unayoishi ni ya kwako peke yako,maana baadaye zisije kuwa lawama kwamba fulani anapenda pesa,hapo usipofikiri unataka mtu afe?maana na kweli njaa imekaba sana mtaani,watu wanapendeza,wanakunywa na kusaza lakini wana taabu mioyoni mwao,pengine ikiwa ni mapenzi ama ni namna ya maisha yalivyoandaliwa.

Katika maisha yako kuna mengi sana,itafika kipindi utasema sasa umekuwa,hata kama ulikuwa unajiona umekuwa,maana kuna wengine wakifanya maksudi na kuona hata aibu wa wakifanyacho,hata kama ikiwa sawa ni kutafuta pesa,lakini namna nyingine ni kutafuta pesa kwa ajili ya kuzikwa,naogopa kuwa Malaya wa maneno na mwisho wa siku wakaielewa wachache,kataa kupoteza muda wako,maana kwa lile lililopita liache liende,hakuna zuri moja katika dunia zaidi ya kile akionacho mtu,pengine wengine wakafikia hadi moyoni,unaweza kukutana na maneno mengi sana hata katika mitaa hiyo ni namna ya kukupanua ubongo,yaani experience,kwa vile mtoto alianza kusikia na atasema,wakubwa wakisikia huwa ni siri daima.

Pigana maisha ni magumu sana,napigana na ikiwa kwa kila namna,,pigana sana wanadamu hawana hiyana,maisha haya ya leo unaweza kuishi kesho na kusema unaishi maisha ya jana,yanakuja mengi sana mengine yatasemekana kumwachia maulana,tutaona mengi sana kwa kuwa bado sisi ni vijana,wazee wetu wametufundisha vile ilipofika,ni wakati wa kutumia kijiko kujaza pipa kipindi cha masika,utake usitake vyote vimekwekwa uvunguni sharti ya kufurahi ni kuinama.tukiwa kama wote vijana tuombeane kheri haya maisha yasije kutuendea mlama.

):-Benson G. Makaya

KUKOSA SIO TATIZO..

Tatizo ni kwangu maana hata muda bado unazidi kwenda,nimekosa leo nikitegemea kupata kesho,ikiwa kila mtu ana kipato chake,kwa upande wangu sijapata na ikiwa kwa upande wangu ulio kwako umepata basi uhaki kuisubiria ahadi yako kama vile ninavyoisubiri,matatizo ni namna ya kuweza kutafuta,maana kama hautafuti kwa nini una matatizo?hapo ndiyo utasikia wakisema lazima kuna mchawi hapa.maisha mchawi ni wewe,hakuna mlinzi mzuri wa mwili wako zaidi ya wewe mwenyewe,hivyo ukishindwa utajiletea matatizo,tena ‘matatizo’ ni kama ‘maisha’ maana yenyewe yana mazuri na mabaya.

Duniani ndiyo mahala pa kuishi,utasikia ikisemeka kwamba duniani maisha magumu sana ,sasa wapi rahisi,unapoona nyuki wanakukimbilia na wewe kimbia,kwa mfano wa kuku anapotakwa kuchinjwa siku yake inapofika,maana siku yako ikifika hapo utajua tatizo,tena yenyewe huwa hayana hodi wala kalenda labda siku fulani yapasa kupumzika ili kusherehekea,maana itakuwa imepatikana.pengine matatizo yako ikiwa kama ni raha ya mtu mwengine,wewe unacheka wengine wanalia.hapa ikiwa lazima ujue umekosa nini.

Tatizo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu ikiwa ameamua kuishi,wengine wanakata tamaa kwa kuona maisha magumu,kama wale wanoenda shule na kuacha,ya kuwa shule ngumu,na bila kugunndua baadaye itasemeka ni kwa sababu shule haikuenda.maisha yenyewe ni shule,matatizo hasa ndiyo yanayomfundisha mwanadamu,kuna mengine yale yanayokosekana yakaonekana kama na yenyewe ni matatizo,sasa kama yakija na yenyewe kwa matatizo yake si utakata roho kabisa?labda ikiwa ni furaha..,maana kama kile kilichokuwepo kimekuwa tatizo basi hata  kisichokuwapo haina haja ya kukisumbukia maana tutaongeza matatizo tu.

Thursday, August 16, 2012

AHADI


Kama unavyoweza kusema utarudi tena,ikiwa umeahidiana kitu ki maongezi pengine hata vitendo,au vile jana ulisema na leo imetokea basi hakika na kesho inapaswa kutegemewa yakuwa dunia ni duara,pengine Mungu angewaahidi wana wa Israeli kupitia musa wazungushwe hata pengine wangemsaliti kwa asilimia kubwa sana,maana wengine wangejifanya wanajua kurekebisha bila ya kuhofia  yatakayo haribu kwa vile kiongozi alivyo sidhani kama ahadi zinabadilika zaidi ya kutokutendeka,maana hapo utabadilishana ya moyoni,muda unayake kaa ukiwa na subira ya kile ulichoahidiwa kesho

Hakuna na kuogopa zaidi ya kuamua vile vinavyokuja bila ya ahadi maalumu huwa havidumu,pengine ikiwa ahadi inafikirika kwa siku nyingi sana,pengine uyo aliyeahidi akiwa mwongo  ndiyo vile maana ya kutokutendeka,na kama ilikuwa ni mara moja basi haina haja ya kutegemea ya pili,pengine kama Mungu angeahidi kufika katika nchi waliyoahidiwa,na baada ya kikwazo cha bahari wakadhani sio Yule mungu musa aliyemtuma kuwafikisha wanawe mahala,lakini walivuka na kufika pale,tena waliandaliwa,uliye na imani tofauti fikiri hili ni kama neno.ahadi hata kama ni tofauti lakini ziwepo uzikute upande wa kutumia iache subra yako.

Kesho ndiyo siku njema mahala hata nilipo ni zamani,kila dakika ya kufikiri inakwenda bila hata ya kudhani umeahidiwa nini,pengine ahadi yako bado hazijatoka au yapasa kuomba tena na bora kesho ije maana yale yote ya jana yanategemeana,sidhani kufika kumi bila moja iliyopo,pengine mungu amekuahidi kitu kimoja tu pengine kila mtu akamshukuru mwenyezi Mungu vyema akafanya hivyo pengine utende yanayostahiri kwa kila mmoja wetu ili usiweze kugombana kwa zawadi zitakazo kuja kwa ajili yako ikiwa zilikuwa na ahadi.

KUWA HURU..


Kuwa na uhuru kunakufanya uwe na mafanikio,yaani ukiwa na uhuru wa maamuzi na kutenda,pengine kila mtu anatenda yake,hata Yule unayemwita mwehu naye anatenda,pengine hapa ndiyo tukafikiri nakujua kuwa  palipo na mwanadamu panahitaji akili,yaani fikra zilizotimia,ikiwa inajua nini kile inachokifikiria,pengine tumekuwa na uhuru tangu mda mrefu na tumeshindwa kufanya lolote,sisi ni wapumbavu..yaani hatuna akili maana tuliyotenda ni sawa na bure,uhuru wa bure,tena ingalikuwa wanaotupa uhuru hawatukufahamu  tungalikuwa  udongo kabisa.

Sijamwona huyu wa kunitisha maana mengine aliyasema baba,ndiye aliyenipa uhuru wa kuishi hapa duniani,mengine wala hata si haba maana hata watoto wadogo wa sasa wanayo.waswahili tunasema samaki mmoja akioza wote huoza,tukisahau walikula mpaka maiti..au mtoto wa nyoka sio nyokaa..?uhuru mwengine unatia raha sana,maana unaweza ukajiona mfalme lakini ukafika muda uliopangwa ukahisi njaa,pengine wengine wanapitisha hata siku ngapi,pengine wakiwa na ufalme wao ama vile kwa ukwabela wao,huru ikiwa inahitaji kutokea maana kuna utofauti mtatu,ama mbili kubadilishana na moja au moja kubadilishana na kila moja nyenzake,kuwa huru kuelewa..

Ilipofika siku yake ilitokea,maana wale walio na mafanikio katika mambo yao wataelewa,jinsi vile namna waliweza kukumbuka mpaka kufikia hapo,uhuru hauhusiki na utumwa.ukitakiwa kuwa mtumwa basi unatakiwa utambue mafanikio yako,sasa ujue kwa kutumia akili yako,maana mwishoni tutaona matendo yako,baada ya kifo kuna maneno machache tu..kama tungalikuwa huru kufungua mbingu basi ingeeleweka kwa uchache wake.
kuwa huru katika maisha yako maana kile kilichoandaliwa kwa ajili yako kitatimia

Wednesday, August 15, 2012

MZAO..


Omba kuzaliwa lakini sio kuzaa,pengine ni wazi inahitajika kwa umri fulani kupata japo mwana,lakini ni lazima tuangalie na kizazi kilichopo,maana kama wangu angekuwa amechelewa kidogo basi ningemuombea uhamisho wa kuzaliwa mbele kidogo,kwa maana kwangu haikuwa bado.unaposikia bilabila ni ya hakuna,sasa kama vizazi vipo na inasemekana kuwa hicho kizazi kijacho kitakuwa na hasara sana,ningependa kufahamu hatari yake lakini kumbe ni ile ile namna ya kutaka kutokufanya,maana hichi kilichotabiriwa kuwa kibovu kimekuwa kizima ni kwa sababu wale wazima walikuwa wakifikiria hasara.

Ikiwa mnyama anahitaji kupata mzao mzuri ni lazima awe anakula vizuri na kuudhulia maswala ya afya,pengine wazee wa zamani ni wazi walikuwa ni watu wa ajabu sana,sishangai ngozi nyeusi kuitwa nyani,kwani unapochelewa kuingia shuleni ni viboko na wala hatuwezi kusema wewe sio mwanafunzi,kwani hata pengine baadaye itakuja na kuulizana ‘una mtoto gani,ama vile ana umri gani?’hapo ikisahaulika kama walishamfukuza darasani kwa kuchelewa.na baadaye yakitakiwa majibu kupitia kile kilichokifanyika

Hakuna mzao mbaya bila ya mtu kutokulitumikisha tumbo lake,pengine inapaswa hadi kulala lala chini ali mradi  usisikike..kama nyoka vile.maana kwa muda uliopo sio lazima ya kusema kwamba bora angetangulia fulani,maana hii au hawa wa leo wamekuja leta ubovu,hapa nikikumbuka ya kwamba mti haupewi lawama bila ya jua,maana hata lisipokuwepo litasinyaa tu,pengine ikiwa ni mzao wa mti mwema

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...