Wednesday, August 15, 2012

MZAO..


Omba kuzaliwa lakini sio kuzaa,pengine ni wazi inahitajika kwa umri fulani kupata japo mwana,lakini ni lazima tuangalie na kizazi kilichopo,maana kama wangu angekuwa amechelewa kidogo basi ningemuombea uhamisho wa kuzaliwa mbele kidogo,kwa maana kwangu haikuwa bado.unaposikia bilabila ni ya hakuna,sasa kama vizazi vipo na inasemekana kuwa hicho kizazi kijacho kitakuwa na hasara sana,ningependa kufahamu hatari yake lakini kumbe ni ile ile namna ya kutaka kutokufanya,maana hichi kilichotabiriwa kuwa kibovu kimekuwa kizima ni kwa sababu wale wazima walikuwa wakifikiria hasara.

Ikiwa mnyama anahitaji kupata mzao mzuri ni lazima awe anakula vizuri na kuudhulia maswala ya afya,pengine wazee wa zamani ni wazi walikuwa ni watu wa ajabu sana,sishangai ngozi nyeusi kuitwa nyani,kwani unapochelewa kuingia shuleni ni viboko na wala hatuwezi kusema wewe sio mwanafunzi,kwani hata pengine baadaye itakuja na kuulizana ‘una mtoto gani,ama vile ana umri gani?’hapo ikisahaulika kama walishamfukuza darasani kwa kuchelewa.na baadaye yakitakiwa majibu kupitia kile kilichokifanyika

Hakuna mzao mbaya bila ya mtu kutokulitumikisha tumbo lake,pengine inapaswa hadi kulala lala chini ali mradi  usisikike..kama nyoka vile.maana kwa muda uliopo sio lazima ya kusema kwamba bora angetangulia fulani,maana hii au hawa wa leo wamekuja leta ubovu,hapa nikikumbuka ya kwamba mti haupewi lawama bila ya jua,maana hata lisipokuwepo litasinyaa tu,pengine ikiwa ni mzao wa mti mwema

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...