Friday, August 10, 2012

TEGEMEO.


Yote ni ya Mungu haina haja ya kumwachia mengine,eti haya ya mungu ya shetani yako wapi?tegemeo lako likidondoka angalia kwa kushikiria,siku hizi wanauza watu,yaani uwe mtoto,mkubwa,bila kujali jinsia,ukitegemea sana ya mbele unaweza kufa maskini,maana haukufanya zaidi ya kutegemea,hakuna mjinga anayejihukumu kwa zuri lake,maana makosa anayaficha…makosa ndiyo mafunzo,unapomwambia mtu unategemea nini namatumai ya kuwa na wewe ulikuwa unategemeo lako,maana kama mko zaidi ya mmmoja mtatuletea mategemeo yenu.

 Mazuri ni mengi ndiyo maana kila mtu akawa ya kwake,bila hivyo tungemiliki nafsi moja,na ikiwa ni hivyo basi jaribu kutegemea kitu,maana hata ya kukumbusha tu.pengine imekuwa tofauti sawa na pale ukaambiwa mjini kuna magorofa na kufika mjini kuona nyumba zimepandana,ukiwa na mategemeo ya kiasi fulani huleta faida ya kile ulichokitegemea,maana matokeo yakiwa tofauti na mategemeo hapo lazima kuna mwingiliano,ikiwa mtu hajajitambua au kifaa hakijakaa mahala pake.

Pengine iangaliwe usije kufanya yale yaliyo ya watu,maana kwa kushindwa kutegemea au kutegemea tofauti maana ukisema nzuri bado itapasa kuifahamu na mbaya iko wapi,ili inapokuja labda ufurahie yatakayo kuwepo kwani hakuna namna ya kubadilisha zaidi ya vilivyobadilishwa,maana mategemeo ni namna ya vile mtu alivyofikiria na kuona ile itamfaa ya kuwa ilitokea baada ya yeye alipofanya.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...