Friday, August 10, 2012

NANE NANE


Sitashangaa kusikia moja moja,maana pengine imekuwa ni kama matokeo tu,tunapoonyeshwa hatuoni kwa kusema ona,maana na macho na yenyewe lazima yaambiwe ona,ikiwa kila sauti yanasikia maana tumeona vitu vya ajabu sana katika mikusanyiko yenu,mikutano ikiwa nane inaashiria kuendelea kufika kumi,tujue ya saba imetoka wapi basi.wananchi na nchi yao hawawezi kuwa wapumbavu kwa kushindwa kuelewa wanachoonyeshwa,hapa wanahitaji kuelekeza ikiwezekana kupewa semina,sijui tunaishije bila semina maana ndiyo yamekuwa maisha yetu,sijui unajifunza nini humo,sijui ndo hivi vya semina ama ni katika kufanya biashara.

Siku ikiwa ni ya nane ni kwa sababu ya saba jumapili,ndiyo maana ukasikia sabasaba,hawa watu wanapenda sana kupumzika ikiwa ni siku yao ya kuonyesha,si wanauza..!wewe ndugu yangu umelima lini jana tunasikia unalia njaa?au nini nisaidie ndugu yangu maana kila kitu siku hizi ni maonyesho ya sabasaba,wapeni watu uzalendo wa kuifikiria siku kuku,pengine mtu akiwaza shari kuzidi heri,sikunyingine zinakuja maana mpaka kumi kumi.ikiwa huduma zitaonekana kuwa duni.

Muda unatoka tofauti ya vile tulivyofundishwa,maana na wenyewe wanahitaji kufundishwa,kwa hilo ukiamua kusema kilimo kinaanza sio kama uzamini wa simba na yanga,hapa ni zaidi ya ‘madaruga’ na ‘mabarugaja’,ni zaidi ya kombati siku yake ya kumi inapofikia,maana hapa tutasema dunia imejaa mengi kwa bila kufikiri yale yamoyoni umeyaweka sana akilini,inaleta matatizo kubadili maana kwa kuonekana ikiwa kama ushahidi,angalia namna ya maisha uliyochagua kabla siku ya saba haijaisha maana hii ya nane utaingia shambani.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...