Monday, November 12, 2012

NGUVU ZA LAZIMA....


Ikiwa mungu ni kila kitu na wa kila mtu,mwanadamu amepewa uwezo wa kuweza kufanya maisha yake,kufanya maisha yako ikiwa siyo kujaribu,yaani kutokuwa na uhakika wa kile unachokifanya na baadaye ukaja muda ukasema unajaribu,hata ingali ikafika kipindi wakubwa watalazimika kufanya vya watoto na hii ni kwa sababu wakubwa waliwaambia watoto kwamba usifanye kile cha wakubwa.katika kufanya maisha hakuna kujaribu na ili ueleweke unaishi ni lazima kutumia nguvu za lazima.na wala siyo lazima kufanya ulazima huo ikiwa haina ubishani katika kila mtu anapofanya maisha yake

Haikuwa na maana kwa mtu mkubwa kavaa nguo za watoto,maana hii ni fashion,ama ikawe jitu kubwa linataka sifa za kitoto.maisha hayana ngoja wala subiri,leo ukiwa mahala fulani fikiri kama na jana ulikuwa hapo,jua mwisho wa maisha ni pale utakapo kuwa hau ishi tena,hakuna mtu wa kuweza kuishi maisha ya mwenzake,ikiwa chaguzi la mtu ili kueleweka ameishi siyo lazima awe na kile wewe unachokitaka,unaweza kutumia nguvu kulazimisha kuota ndoto uliyoota jana ya kuwa ilikuwa nzuri sana na kujikuta umechelewa kuota ya leo,unaweza sema yote hayo ya mungu ya kwako fikiri, fanya yanayotokana na maamuzi yako

Kumbuka umeletwa duniani ili uishi,umeweza fanya mengi kwa nguvu zako na baada ya kumaliza akatajwa Mungu hapo ikiwa uliweza,toa nguvu zako..jiamini wewe ndiyo wa kufanya lile la lazima,ikiwa furaha ya maisha yako ni wewe mwenyewe,hauwezi kunywa pombe na kuiomba ‘KILEVI’ kikuleweshe kidogo,unasahau pale unapoanza na kukumbuka mwishoni kwani utamu wa mwanzo huonekana pale nguvu zinapoisha,siyo lazima kulima ikaeleweka unanguvu nyingi na haujaja kujipaka rangi ili kuonekana umpendeza,maana utapaka rangi zote na kujikuta umekuwa na rangi ya kopo la kuchanganyia mara nyingi huwa inakuwa haieleweki.

NI WAZI KILA MTU ANAJUA,HIVYO KAMA UMESHINDWA KUELEWA VINGINE  FANYA UNAVYOJUA WEWE ILI KUSIWE NA LAWAMA.

No comments:

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...