Sunday, July 15, 2012

KIZUNGUZUNGU...


Kizungu zungu kinachanganya sana,maana kwa mtu kuwa mkubwa naye anatakiwa aongee kizungu,ndiyo hapo watu wengi hupata kizunguzungu,kizunguzungu sio ya maana ya kuchanganyikiwa,heli ingekuwa kukuchanganya kuliko kizunguzungu,maana itafika mwisho uelewe kwamba kinachoitajika ni kizungu,sio kuzunguka zunguka.maisha yanaweza kukuweka ukawa katika namna ya kizungu zungu maana yenyewe hupenda kwenda na kurudi na Yule anayeyazungusha ni wewe,sasa ikawe umependa kuzunguka sana lazima ujue kizungu,hapo usije kuchanganyikiwa kwa mizunguko ya maisha iliyopo..

Hakuna kile kilicho cha zaidi,zaidi ya mtu mwenyewe,unapoamua kuanza ndiyo pale mwisho wako unaweza kujulikana,maana mwishoni tunataka kuulizana..wewe umefanya nini,pengine hapo ndiyo tukajua kama kizungu kinafahamika,maana zile YES au NO utaona zikitamkwa kwa namna tofauti,bado hapo tuleteane kizunguzungu maana sio wote watatuelewa,na hata kwa mmoja usitegemee kueleweka  mwanzoni,maana katikati kuna miiba,na safari bado haijaisha hii.

Leo tumetawaliwa na lugha tofauti sana,wale wa kizungu tumejitawala kwa lugha tofauti sana,haki ya mtu kujitawala.jitawanye mwana dunia ni yako..hizi ni kauli chache kwa baadhi wanapoweza,maana unaweza kufanya jambo kwa kurudi nyuma,hapo ukiwa hautembei,hata kama kutembea ni kwenda mbele na nyuma,basi chagua kutembea nyuma,hapo utaona namna ya kizunguzungu,ikiwa ni kurudi nyuma..kwa kushindwa kuelewa  maana tu.maana unaenda enda tu,kama unakizunguzungu vile.tunagalie haya ya leo kwa maana ya kesho,isije kuwa ya leo ya leo tu..

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...