Saturday, May 18, 2024

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2:   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...

Saturday, March 30, 2024

ELEWA 2

 

Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa kuelekezwa,kimfumo kumtafuta mtu kwenye kundi ni ngumu,ili kutofautisha kama kuna mwizi,malaya au mlevi ni kuangalia alipoiba aliekea wapi maana vyote vinaweza kuwa vya mtu mmoja.

Sifa mbovu inayotembea ni sawa na rungu la kichwa ukiwa usingizini, katika miliki matendo mabovu yamekuwa yakitendeka bila woga kuliko mawazo ya mazuri,anayekusifia mazuri hadharani anakusubiri utoke,yule asiyekusifia ana ubaya wake mwingine wa kuelezea.ukigeuka watakwambia hawajakuita na hata wakikuita hawana cha kukwambia.

Kuna namna ipo umefanana na wazazi wako,hata isipokuwa sura basi hasira,tabia wengi wametokea utotoni usimlaumu mtu kwa  kuwa malaya vile unavyojisikia kunywa pepsi mwingine coca,vingine vipo ndani ya damu hivyo tembo akinya sogea mbali pengine uchafu utakumwagikia alafu iabidi uelewe kufuata yako.

Kuna muda huelewi,yaani hata nilichokiandika hauelewi,tatizo lisije kwangu maana ulivyovijaza kichwani mwako vyaweza kuwa kinzani na hivi,nikawa naandika kwa kutumia wino mweupe.kuna mmoja alisema yanatoka popote bila kujua yametokea wapi,ukitaka kupaa kuwa na mahusiano ya karibu na ndege.Usipojua yanatoka wapi jaribu kuwaelewa ndege kwanza.

Watu ni zaidi ya chochote,yoyote yule umwonaye.hata sifa zangu hakuna nzuri imekuwa kwa mwengine,maana kila mtu ananjia yake mafanikio sio utu,ukitaka pesa watakutesa.unapotaka kunielewa isiwe kwa mlengo wako,mtu akitaka kukuelewa asikuelewe anavyokuelewa Ukiishi usimwambie na mwenzio baadaye atajiita kuwa mshauri.

ELEWA 1

Usidharau upendo unaoupata,sio kila kinalengwa kinalengeka,ukiona mchele umeota kwenye maji kuna ardhi chini ,haihitaji nguvu kupanda mbegu,itakuchosha mapema na utapoteza furaha yako vivo hivyo,asikwambie mtu kucheka wakati mrefu wa kununa ni nguvu tosha na ikakupa amani muda wote.

kama hakuna jibu kwanini uliingia kwenye mdomo wa mamba basi utakuwa unaishi nao,kujua kuogelea sio kuitii kiu ya maji ya kunywa,sehemu nyingine za kuogelea kuna mamba,wazee hupendelea sana swimming pool,sehemu za kuogelea ndogo ,vijana hujitupa maziwani na mabaharini na wakifika katikati hushituka na kujilaumu,na huo huwa msingi wa kubomoka.

Kuna maziwa na bahari nyingine zina ghasia sana,utaratibu mtu mmoja lakini wao huwapanga hata ishirini,mawimbi yanatoka popote kwenye mwelekeo,bora swiming pool mawimbi utayaleta wewe.wanasema saidia uendelee na safari,ni vile unatoa dhaka na mchungaji anaenda kununua shamba ili alime apate chakula cha kuuza na familia.

Elewa kwamba sio yote unayoyaona lazima uyaelewe,hata kama umeyasoma sio lazima uyaelewe,elewa wengine wa kuwaacha,kataza moyo wako kushikamana na matendo,Elewa duniani kuna watu watataka kwa lazima kufikiria tofauti ya wewe unavyofikiri ili wao kuonekana tofauti.

Wednesday, January 24, 2024

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO: Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahal...

Makaya's Forum: HASIRA YAKO

Makaya's Forum: HASIRA YAKO: Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinak...

Tuesday, January 16, 2024

HASIRA YAKO

Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinakupeleka,binadamu tupo tofuti,mmoja hali nyama ya mbuzi kwa kuwa inamtoa vipele mwengine hali nyama ya nguruwe kwa sababu ya dini sasa nikikasirika usiniulize nimekasikia nini,nina mengi.

Kasirika,usikarike pasipo na sababu.upumbavu wa mtu mmoja usikufanye uvunje simu na mwengine kufikia kumkata mtu panga.angalia unapokasirika sauti yako ya ndani inakwambia nini na kabla haujatenda kwa kutumia kiungo chochote cha mwili yakupasa kutafakari,maana kuna wale wenye hasira za ndani(chuki) hawafanyi mambo yao hadharani.

kama ilivyo katika michezo mmoja akamchezea rafu mwenzake basi wanamichezo waliiga kwenye maisha,na ndiyo maana unasikia michezo haiitaji hasira,ukisusa wenzako wanakula na wenzako huwa wanakula mpaka baadaye ukakitamani tena hicho chakula,kasirika vizuri.

Dunia hadaa utakasirishwa wakitaka kujua maamuzi yako,ukishajua umekasirikia nini maamuzi yako yawe tofauti na hasira zako kwani kweli maisha yana mengi lakini kuna mengine sio ya kukasirikia fikiri mtu anakasirikia mafanikio yako na atayekumbatia maamuzi ya hasira zako yampasa kuwa yeye.

ISHI NA YAKO

Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahala fulani,tambua maisha yana stepu,uliyopo sasa mwengine alipita juzi ukicheka leo mwenzako kulia ni sawa na kulia wakati mwenzako anacheka.

Usibabaike na waliowahi kufikia ukitakacho,tambua muda wako ikiwa unajiandaa jiandae vyema ili ukikosa isiwe lawama kwa wengine,maana imekuwa mmoja akishindwa akatoa sababu za mwengine kumuangusha.

Usifikiri ni raisi kukaza jambo,kuna mengine yanakaza mpaka kufungua inakuwa kama ni kukaza,ujiandae vyema maana kuna vilio,maumivu yasiyo na machozi na hata usumbufu usiohitajika.yatambue magumu yako na jipe muda kuyatatua ikiwa humu duniani wote mpaka muda huu tunatafuta maisha.

Kheri udongo unarudi utokapo maana ingekuwa foleni kubwa barabarani kwa kuwapa heshima wajionao miungu,usifikiri wakati wa magumu peke yake mwishowe ukawapa lawama watu wasio husika na maisha yako,tambua nafasi yako si ile aisemeayo mwengine,watu huwa wanaongezea kwa kile ulichonacho.

Monday, October 9, 2023

Makaya's Forum: NAONA

Makaya's Forum: NAONA: Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni ...

NAONA

Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni moto na unaunguza,Naona vingi ukipata uelewa ntakuelewesha.

Naona wamefunga milango wakijua upo nje,wamefunga njia ikiwa bado haujapita,wanakusema unakonda kwa kukataa kunywa uji,naona ukisoma herufi bila ya kuelewa,umeanza kuita mma ukijua ni uhai,naona chuki juu ya moyo mkunjufu,Subiri ukipata uelewa ntakuelewesha.

Naona hujajua kama sufuria sio kikombe,hujajua mtu anayesubiria hakupata hajapata sifuri,usikimbilie kuendesha vitakavyo kuendesha,subiria kupandishwa basi likisimama utashushwa,Unapokula usijichafue sana meza wapo wabaya watu wanaotafuna vya kumeza.

Naona unaanza kuelewa ya msingi,ukitaka kujisaidia waogope watu na isiwe kwa chuki ,kama umekuwa jua safari unaiweza na unapoelekea naona safari ndo inaanza,Naona unashindwa kufanikiwa kwa fitina nyingi,vita zipo nyingi kaa mbali na maadaui,binadamu yoyote anaweza kuwa adui bila hata wewe kutaka,naona unakuwa msuruhishi mbele ya ndugu zako na sio kuwagandamiza.

Kesho naiona tena,naliyaona ya jana yakanipa majibu ya kuwa mtihani ni ule ule.naona yake akae nayo yako baki nayo mwenyewe ili kutokuchanyikikika,Naona unakanyaga maji na hakuna sehemu yenye moto ,Naona nisikuchoshe Sali sana kaa mbali sana na ndugu msumali.

Thursday, October 5, 2023

NEEMA YA MUNGU

 Neema ya Mungu haipangwi na mwanadamu ,maana siwezi kuomba na kutaka nijibiwe kesho ama muda ule nitakaotaka ikiwa naamini Mungu anapenda maisha yangu na yupo bize kuhakikisha shetani hanichukui moja kwa moja,

Ufahari na mafanikio  unaweza kuwa hitaji la kila mmoja lakini vitu hivyo vinagharama na unaweza kulazimisha kugharamia ukawa navyo lakini ukakosa namna ya kuendesha na kufurahia uliyochonacho,ikawe muomba jiwe akapewa mkate.

Namshukuru Mungu hata nisingekuwa hapa,naishi vile Mungu ametaka na ifike kipindi nisisahau wala kudharau kusali na kumwomba kwa kuwa yeye ananipenda,anabadili kile kitu kinachosumbua nafsi yangu ,anajua ninachohitaji na muda wa kunipa.

Najua maisha yangu hayajabadilika hivi hivi bila neema ya Mungu,pale ninapo muomba ananipa,anabadilisha mazingira.Hata kesho sitasimama peke yangu maana ndiyo umenifikisha hapa nilipo,

Maombi mengine ukatizwa na hofu na kuzuia neema zisikudondokee,namuomba Mungu nifanye tofauti na hofu ilivyo iwe kutaka,kuendea na kukipata kukiwa na maono juu ya kile ninachokihitaji,

Ndoto hata ikifeli moja ntaota tena maana neema yako Mungu haina muda kamili,muda wa kupata kitu zaidi kile mtu usichokidhania.

Wednesday, May 27, 2020

Makaya's Forum: YAFANYE MAPITO KUWA ELIMU.

Makaya's Forum: YAFANYE MAPITO KUWA ELIMU.: YAFANYE MAPITO YAKO KUWA NGUVU INAYOKUSUKUMA KWENDA MBELE UKITEGEMEA KUISHI NDOTO ZAKO NA SIO KILE UNACHOKIOGOPA NA KUHOFU,IKIWA WATU WENG...

Tuesday, April 23, 2019

Makaya's Forum: KATAA

Makaya's Forum: KATAA: unaweza ukawa unakataa mazingira uliyonayo,ukajikataa,ukakataliwa ama ukakatalika  hiyo yote ikaonekaa kwa kuwa maisha yana msukumo tofaut...

Saturday, April 20, 2019

BINADAMU UNAPOJIULIZA(usimwachie Ulimwengu)


Najiuliza umeniuliza kwanini Sitoi salamu nami huwa najiuliza pia kama huwa unaipata salamu yangu,ikiwa ubongo wa mwanadamu wa kila aliyeumbwa una swali la kujiuliza jiulize unaelekea wapi maana kila siku zinavyokwenda ulimwengu unaelekea na kuzidi kutoa maswali yanayoendana na technolojia ambayo haikukupa misingi yenye mizizi ya kina katika kujua mambo yaliyo duniani yanayoendana na maswali hayo katika kukabiliana na maisha ulimwenguni. 

Jiulize kama umeshawahi kujiuliza kwa nini unafanya kile unachoweza kukifanya ama kwa nini unahitaji kufanya kile ambacho unahitaji kukifanya?je pengine ukifikiri  kuna kuwa na uhakika wa kupata majibu ya maswali hayo au njia na majibu ya maswali hayo?maana aina nyingi za majibu yanayotokana na  kuangalizia yanakuwa hayana maana iliyokiundani pale inapokuja mtoa majibu anapoangaliwa kwa umakini zaidi, utekelezaji wa waliotoa majibu huelekeza swali hilo lilimlenga nani,ikiwa kila mtu ana mtihani wake hivyo hata majibu ni tofauti pia.

Nimekuja kuishi duniani hivyo nina kila sababu ya kufanya hivyo iliyo vyovyote ili iwe, niishi. kutangulia sio kufika lakini sio katika kifo na hii mara nyingi hunipelekea kujiuliza naishije ama ntaishije ? sasa hili ni chaguzi ukizingatia Moyo nao hutaka kuamua yake pindi majibu yanapotoka hivyo bila kuuhusisha moyo wangu huwa nayavumilia majuto ikiwa pia nazingatia na muda nilioanza kupata wajukuu na kusoma hali zaidi kupitia hapo, 

Kama ndugu yangu pia una jiuliza swali kama hilo pia basi jaribu kuangalia na moyo wako unasemaje ili majibu yako yakahusishwe na wewe binafsi.Na inapofika kipindi humwelewi mwenzio ni bora ukauliza au ikiwa unataka kuelewa jinsi unavyoelewa basi kaa kimya maana mengine yanakuwa siyo yako.

Maisha yana mengi ni mtihani hivyo maswali mengine siyo yako ukiyajibu unakuwa kama unatumia akili yako vibaya,Kama utapenda kuyajibu na kuona umepata zaidi basi Mwalimu(Ulimwengu) ndiye atakayesema kweli kuzingatia na muda na ujue binadamu ameumbwa kupambana kila siku, 

Usijali kama swali la jana limebaki kuwa swali  la nyumbani la leo inawezekana leo kulikuwa hamna swali pia jawabu ni kujipa moyo na kusonga mbele kwa kuangalia yanayofuata.

Friday, April 19, 2019

UNAPOWAZA

Eti kuwaza sana ni vibaya,nawaza sana nakuwa na mawazo nawaza sana yaliyo mema nawaza sana kuongeza kupata maisha sio kama ya fulani bali yale niliyoyawazia,wakati mengine yanapita Shukrani kwa muumba hazitaweza pita,Mwisho wa kuwaza unaelewa mwenyewe maana sio uwaze tu hata yasiyo na majibu,

Mbaya katika mtihani ni kuanza na swali gumu kuliko yote  kumi utajikuta umefeli na kuyashagaa matokeo yakakupa mawazo tofauti  yakuwa kabla ya kuingia katika mtihani uliwaza ukitoka utakuwa na mawazo tofauti zaidi ya yale uliyo kuwa nayo sasa,sijui niwaze nini nikufurahishe, nakusema siwezi ogopa ila muda haumdanganyi mwamuzi labda anayeamua akaamue.

Hivyo unachagua wewe,chagua wewe kuwaza nini mengine ni  mazuri asikwambie mtu mawazo mabaya,ni kheri akakuongezee kwenye huo ubaya maana hata moto anaoupata yule anayechomelea na  yule anayekaanga viazi ni tofauti nawaza tu,ukitaka kutokuwaza fanya starehe,ukifanya za kutosha na hautakuwa na mawazo ya kutosha,naposema starehe kila mmoja anayo katika mawazo yake  unawaza kufanya starehe gani nasema hivyo maana kuna kauli inasema maisha ni mafupi sana hivyo inakupasa kuishi kwa thamani,matumizi yako yakaendane na mawazo yako ila pindi unapowaza kinyume huna budi kuwaza yaliyofanyika maana huo hua ni mwanzo wa mmomonyoko wa yale yanayofuata.

ukiwa unawaza yanayofuata ukawa hujui hasara yake maana kwa muda huo yanakuwa hayana mashiko na mmiliki yaani wewe uliyestarehe kwa mawazo yako kabla hujawaza sasa iliyopo ambayo ni baadaye.

Sikuwaza umri ni kama haya makubwa  ninayoyawaza,wala kuna mengine sijawaza lakini yamekuja katika haya,mawazo ukiyaamini,yanakuletea imani yako inachokiwaza hata ukajiandae na utofauti ili kutokuyazidisha yaliyopo,maana nawaza sikufika hapa kama nilivyo wala sikuwa mimi kama nilivyo,sio tu kwa sababu ya nini ama fulani nikiwaza kwa mawazo yangu ni imani maana sikuijua kesho zaidi ya yule aliyeniambia niache kufanya ya kesho kwa kuwa hata usiku wa leo hayajafanyika.

Unapoona mengi kuna mengine yanakuwa sio makubwa yaliyowazwa zaidi ya kuonwa ikiwepo vingine nawe ukawaze hivyo,nikikiona nakielewa zaidi maana nikikiwaza ntakuwa kama nakiona,shida pale nawaza nisichokiona ninapowaza cha kesho na leo sijaimaliza hapa huwa naamua kufanya lililopo bila ya kuchelewa.

Kuna kucheleweshwa lakini aliyewahi kawai kesho ujifunze kuamka mapema ili kuyawahi mawazo kingafu ,maana kama mawazo yanaingiliana basi hata matendo pia,unapokufa wakisema utakumbukwa wengi ni kwa matendo yako,mengine waliyoyawaza husahaurika ,kufa leo uache mazuri yaliyotokana na mawazo yako na iwe kwa faida yako.

Nawaza ni kheri nizeeke muda mwingine ntakuwa nimepita mengi,nisionekane tu kwa mtu anayeona aonavyo bali nikajifiche kwa vile waonavyo,nilikaa na kuanza kuandika haya nliwaza mmoja atawaza yale ni mawazo tu,lakini kwa jinsi navyoona hata yule asemaye naye anataka kuonekana na mawazo bora,kuna vitu Mwenyezi Mungu amekupa na mwengine hana,Kama unaweza kufanya chochote bora fanya katika ubora uwazavyo.


KATAA


Unaweza ukawa unakataa mazingira uliyonayo,ukajikataa ukakataliwa ama ukakatalika  hiyo yote ikaonekana kwa kuwa maisha yana msukumo tofauti na vile inavyoweza kusukumika,upepo  unaweza vuma kuelekea kusini na yenyewe maisha  yakataka uelekeo wa  magharibi  itakuwa na kueleweka vile inavyoonekana uelekeo ulivyo.

Unaweza ukawa umekatalika upande wa kushoto lakini kulia ukafanya kazi na kama vile ilivyo katika viungo vya mwanadamu,wengine wakatumie  kufanya mambo yao kwa upande wa kulia na wengineo  kushoto yaani pande zote na hiyo ikawe ni kulingana na mazingira ya jinsi ulivyoweza kuumbwa.

Unapokataa jambo ni lazima ujue kipindi cha kukubali pengine muda unaolikataa jambo ndiyo muda mdogo wa kusubiri na kupata jambo lingine likiwa ni lile lililokataa  uelekeo ama ni  jipya,yule aliyekataliwa jana na sasa anang'aa ni katika maisha ya mwanadamu huwa yanatokea,

Yote sio ya kumwachia Mungu Mengine hata yeye aliyakataa akaumba Amri ili uweze kujikataa katika nafasi uliyopo pengine ikiwa na mahitaji ya mabadiliko ama vinginevyo,ingawaje yaweza kupelekea kukataliwa na jamii na watu wanao kuzunguka lakini kataa kukataliwa kwa sababu ya maono ya watu,

Wengine wakadhani umejikataa lakini ni namna ya jinsi maisha yako umeyataka yawe,unapokaa chini ona waliokataliwa wakakata kutokukatalika,maana kuna vile vingine hukataliwa kwa sababu anafanya fulani.

Muda mwingine unaweza kudhani hata ulikosea kufanya kile unachokifanya au ulikosea kuoa,ulikosea kununua mashine fulani hata pengine ulikosea kumwambia mtu fulani jambo fulani na mengine mengi.Kile kinachosukuma mwelekeo kinatagemea uwiano wako na ukikataa kwenda kulia na msukumaji anasukuma kushoto basi jua utaenda kushoto tu.

Sio kila sikio linasikia kile chema kinachoweza kupitia mdomoni baadaye,midomo mingine hukataa kutoa tafsiri sahihi ya kile kilichokipokea kwa kuchelewa kufika taarifa ama kukataa kufikisha kile kilichotafsiliwa na kukifikisha kikiwa na maana tofauti inayoweza kukatalika.

Ingawaje hata kukataliwa kuna faida zake pia usijisikie wa chini pale unaposukumwa na mkatazo,kataa wewe kabla hujakataliwa,yule ajaye kakukataa atapata sababu baada ya wewe kujua kujikataa kwa faida.

Usijisikie hali yoyote katika kukataa,kukatalika,kujikataa ama kukataliwa pengine fikiria matokeo yake kwanza na ukajua leo yangu iliyokataliwa ni Nuru yangu kesho na hata kama kesho  yako inaonekana kukataliwa kataa mawazo ya kuona kukataliwa.


Sunday, March 24, 2019

Makaya's Forum: BADILIKA.

Makaya's Forum: BADILIKA.: KUNA KIPINDI UNAWEZA FIKA NA KUSHANGAA NAMNA YA JINSI MAISHA YAKO YALIVYO,YAKIWA YAMESIMAMA AU KWENDA VILE AMBAVYO HUJATEGEMEA WEWE, KUMBUK...

Friday, November 18, 2016

SHIKA YAKO

Kamilisha mipango yako ukitilia maanani kwa kile chochote ukahitaji kufanya katika namna ya kukataa kujilaumu na kukwepa lawama,Utapatwa na mshangao kwa kuona Yale yanayotokea halisia sio kama vile ulivyofokiri, ukiwa na fikra zilizochanganyika na Mawazo ya aina nyingi yenye kujua lipi ni tusi na lipi ni shukrani.

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwa Pumzi yako kwa vile utakalo wewe hutimia, nakumbuka mengi machache sio kama ya mwengine, Asante Nimekuja duniani nimekuja uwanjani pengine ni mchezo unaohitaji hasira na nikakasirike tofauti.

Watu wanaona wanachowaza wao juu ya wenzao ni sahihi zaidi, yaani mtu anaamua kumwamulia mwengine kwakuwa tu labda wametofautiana katika hali zao hasa katika uchumi wa binafsi na pengine ikawe ni tabia na kujifanya nafsi ya mtu iko mikononi mwao. 

Maisha hayana uelekezi wa moja kwa moja yakakupa kanuni ili ufanye vile na ukafanane, binadamu tumetofautiana katika hali nyingi hasa ikiwa ya kwako umeyaweza Leo mwache kesho aweze mwengine unayemwona kashindwa Leo,haina haja ya kumsemea ikiwa kinachofanyika sio kosa kwake.

Ondoa wivu na roho ya kukunja katika lile jambo aliwezalo mwengine, ikiwa hujui ni bora kuuliza na kumwacha mwandishi aende na faida zake kuliko kusemea kitu kinachokuhusu wewe na kulinganisha na utofauti wa kile anachokifanya mwengine ya kuwa binafsi huna uwezo nacho.

Leo nikiangalia baadhi ya mambo yaliyoonekana na kusema hakuna aliyekamilika katika dunia hii yenye mengi, watu tumetofautiana chaguzi mmoja akaona kibaya ni kizuri  na mwengine akaone kizuri ni kizuri hiyo yote ikiwa ni kutaka kuona mazuri na kuukataa uhalisia, au kuukubali katika namna yake. 

Uhalisia huja katika pande zote lakini binadamu uufanya uhalisia wake pale anapopendezwa nao yeye, ni kheri kukaa kimya kuliko kusema kitu ambacho hakiwezi kufutika maana na kuleta uhalisia tofauti, kwani yanapokuja mabadiliko fitina na uwongo uliokithiri unaweza kuharibu picha na mtazamo wa maisha yanayokuzunguka.

Sibishani na mtu ili akapata faida,aliyetaka kuelewa aliuliza mapema kile kinachohitajika kufanyika na kikafanyika , hakuna haja ya kulazimisha kujulikana kama unajua na wakati haujui, anayefanya jambo moja huacha kutokana na mtu mwengine karibu kufanya jambo lile lile, na aliyeamua kufanya jambo hakatazwi kwa maneno ama kwa  kile kilichofanywa,na akiacha isiwe kwa maneno maana kuna binadamu wanajua ya wenzao kuliko wenzao,wakijiweka wao bora zaidi ama tu kukuchafua kwa vile mpumbavu hachagui neno la kukusemea,

Shika yako na mwache mwengine akiendelea zake.

Tuesday, October 11, 2016

KUZA KIPAWA CHAKO NA KATAA KUSHINDWA.

Vitu vinavyokuja kirahisi mbele yetu kama zawadi inaweza kukupelekea katika sehemu nyingi chagua na kuwa na uzuri  katika kila jambo, amua kutoka ndani ya mfuko wa moyo wako na kuangalia nini unataka kufanya katika maisha yako ukitakiwa kuyandeleza maono na mawazo yako.

Usijifiche bali fanya ni lazima kufanyia kazi kipawa chako ikiwa ni nguvu na tabia ya mtu, amua kwamba utajisukuma ili kufika mahali Fulani kwa nguvu zako mwenyewe,

Nguvu ya mwanadamu ni kubwa sana Zaidi ya ufikirivyo kile ulichoamua hakuna mtu awezaye kukukataza, anza kuongeza na kuimalisha malengo yako kwani mafanikio unayachungulia unayachagua wewe mwenyewe na kipaji chako kikufikishe pale.

Kila siku yakupasa kutafuta nini njia ambayo utafika siku na watu wakuulize na washangae umefikaje pale, maisha yanaweza kuwa ni silaha kwa muda mwingine na vitu vingine watu hawafundishwi hivyo sio kila kile ufanyacho ni mafanikio  yakupasa kuwa na nguvu zaidi ya maisha yako yenyewe na namna unavyoyapima mafanikio binafsi, kubali kwamba kuna watu wanaitafuta iyo nafasi uliyonayo, 

Hakikisha unatumia siku yako vyema haijalishi ukiwa na furaha ama chukizo yakupasa kutambua kuwa ni wewe upo katika hiyo hali na nini kifanyike,ukiwa unajua unachokifanya haikupasi kuwa na maisha ya katikati inakupasa kuvuka vizuizi, usijaribu kuacha kupigana na kukata tamaa, jiamini na Pigania Maisha sio leo wala kesho Kwani umekuja kuishi.

Tambua uko katika misheni ambayo inahitaji ukamilisho wako, usijikatae kwa kukosea maana wengi waliofanikiwa wamekosea sana, utajifunza kutokana na makosa bila kujali ni makosa ya aina gani maana mwenye makosa ndiye anayetegemewa kufanikiwa, sema ndiyo kwa kila jambo linalohitaji kuendelea mbele, jaribu unapopata wewe ni lazima utambue kuwa kuna nafasi nyingine katika maisha,

Kwa kile utakacho toa ndiyo hicho utaingiza, usirudi nyuma kamwe muda wa kushindwa ulishapita,kipindi kigumu huwa kinapoteza vipaji vya watu wengi na kujikuta wakibaki wakilalama na kufanya hakuna, funguo ya kufanikiwa ni kujiamini  kujifunza na kutenda kupitia makosa hayo hayo, 

Toa sadaka yako leo  kwa ajili ya kesho nzuri inayokuja na utumie ubongo wako vizuri ili kukuendesha kuwa na furaha na mafanikio unayoyategemea.

Tuesday, September 27, 2016

YAFANYE MAPITO KUWA ELIMU.

Yafanye mapito yako kuwa nguvu inayokusukuma kwenda mbele ukitegemea kuishi ndoto zako na sio kile unachokiogopa na kuhofia,wengi hawafanyiyale wanayoyategemea zaidi ya kile kilichopo pasipo kufikiri ni kwanini mtu anajawa na msongo wa mawazo yanayokataza kuishi ndoto zako.

Labda  kwa sababu ya watu na matendo yaliyopita yanaisumbua roho yako, watu wengi wanaishi wakikimbilia wasichokijua kwa kuogopa nafsi zao kubaki nyuma na baada ya kuangalia wanajikuta walichokifanya kilipaswa kufikirika kabla ya maamuzi ya kutenda, hivyo kukuletea shida katika kufanikisha mambo  pasipo kujua wapi walianza.

Wengine wanaishi maisha yao kwa kujiona, kujiona kwamba ndiye yeye,ukijiona kwamba u tajiri na wakati bado ukihitaji msaada na kuuacha uhalisia, kwamba kila kitu kipo sawa katika malengo na yale unayoyahitaji huku unasahau maisha yanakutegemea wewe, kwa lolote unalolitafuta na lenyewe linakutafuta, ni kama nguvu ya mvutano.

Hivyo ni lazima kuwa nalo jambo, acha kufanya lile lisilo na tamanio kwako na fanya kile unachoweza maana na chenyewe kitafanana nawe, ukitembea sana katika maisha utakutana na kauli ambazo nyingine zinasimamisha na kurudisha nyuma nafsi yako, ikiwa lakini yako utaitumia vizuri ukiangalia ni wapi utawekeza akili yako  na baadaye uyaache maamuzi yako yakikufata sambamba nawe.

Angalia katika njia ambayo unaweza kuyatengeza maisha yako yakawa vile utakavyo kama vile ukaamini kwamba ipo siku maisha yako yatakaa na kubadilika ukiamini unaweza kuyafanya maisha yako katika yale utakayo yakakurudia ama kukupata upya, kama hauna kitu nyanyuka na ukafuate kile unachokitaka.

Hutapoteza kile unachokitaka kipo na kinakusubiri wewe kama bado ulikuwa haujakipata,achana na mawazo ya kilichopotea maana unapoelekea ni mbele kupata maana amua sasa ili watu wengine waje wasome kupitia wewe.wengine wanasema hapana huku wakiwa hawajui kama wanakataa juu ya nini.

Nguvu iliyopo ndani yako ni kubwa,jiamini na safiri na nyota yako.

 

Sunday, September 25, 2016

FANYA LEO YAKO


Kuna Wakati mtu unakuwa na hofu ya kuishi na hali ya kutojiweza na kusema huwezi au kwa sababu ya hali na uchumi wa nchi ulivyo,matatizo binafsi na kukata tamaa,kuwa na tatizo lolote linalokufanya kuhofia kesho yako.

Inakupasa utafakari muda na uangalie ni vitu gani vinavyokushinda kuvifanya na kuvinakili pembeni nakuanza kufanya chaguzo katika lipi lile utakaloanza nalo maana utakuwa umeitumia leo yako tofauti na ilivyoifanye leo yako ikajenge kesho nzuri na ukitambua nini kazi ya maisha yako kama hauwezi kufanya mda flani basi japo kidogo.

Ufikirie ni nini maisha umeyaandalia katika muda wako husika hapa duniani,unaweza kujifariji kwa kile unachokiweza kufanya Leo kwa kutofanya na kusema utafanya kesho na usifanye tena,hii yaweza kukufanya usiwe na uhakika wa maisha yako na hata ifike kipindi usiamini kama ni wewe kwa kujiona bado wa jana,

Na ufikiri zaidi ni namna gani unaweza kuendesha maisha yako sio zaidi ya kuishi maisha yao,hii inapelekea na kutokana na  kuhairisha na kufa kwa ndoto kutokana na misongamano iliyopo katika mizunguko ya maisha,

Yakupasa kuzoea magumu kujua kwa nini haijafanyika na sio kulaumu kwa nini ulishindwa kufanya,fanya leo bado haujachelewa usiogope nafsi na macho ya watu wengine wanaokuzunguka,ukijua Leo wewe ni nani ukajua ni namna gani ulivyoachiwa jukumu La kufanya ndoto yako kuwa maisha kwa kuyatekeleza Yale unayoyategemea katika maisha yako.

Katika kufanya Leo yako Leo inahitaji ujiamini,ujisikilize na uisikie ile sauti inayokwambia kitu ndani ya moyo wako,yaache Yale yaliyolegea peke yake ukiwa umeyatilia maana ukiyaacha ndiyo utajua wewe ni nani maana kile kilicho na penda kitaashiria upendo ndani yake na kuonekana juu yako.

Usitumie muda wako kubishana na mtu yeyote hasa katika mambo yasiyo na msingi,kujua jambo la msingi ni kujua kile unachokihitaji,pengine usibishe usilolijua ,kuna vitu vingine unavichukua katika maisha yako na kuishi navyo lakini inapofika kipindi Fulani ni lazima kusema imetosha,

Ikitosha huwa inatosha,ni kama kushiba ilivyo tofauti na kuwa na njaa,maana ukishiba ukala tena basi kuna shida mbele yake,inaogopesha kuendelea na maisha huku fikra zako zikiwa zimezungukwa na hofu,wale watu wote wanaokuzunguka ni faraja tosha katika njia ya maisha yako kupitia kile unachokisema,unachokisikia na kukitenda juu yao na wao juu yako,

Ukiwa popote na nguvu ya kufanya lolote msingi ni kujiruhusu we we mwenyewe kufanya kitu Leo sio kwa kufikiria kilichokuwa kinafanyika zamani au wakina Fulani wanafanya nini.

Maisha ni kukua,kama hakuna kukua ni lazima kufikiri nini kinasimamisha pale kunapokuwa hapakui,Ndio maana yakuwa na kesho ambayo yaweza kuwa leo yako,Usichanganyikiwe kwa vile ulivyo na kile unachokifanya leo,weka ubongo wako kuwa  ardhi yenye hitaji la kupanda mbegu bora tena tofauti tofauti.

Amua kukua kwa njia na Mawazo sahihi na kufanya yale mazuri Leo tambua kila MTU ana mawazo mengi jaribu kile unachokiogopa na kataa sauti inayokukataza na amini kufanikiwa nacho,kufanya kwa kuweka mawazo mapya yanayoendana na maisha yako ,

Kupenda na kufanya linalotakiwa kwa  kuwa muwazi,mwaminifu na kuishi katika sababu na majibu yako,pale kwenye lawama ukaweka msahama, Nia thabiti katika kila njia upitayo bila kusahau kumshukuru  Mungu pale Uionapo Leo yako.




Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...

POPURAL POSTS